Narcotics Anonymous (Tanzania)

|
Mila kumi na mbili za Narcotics Anonymous (NA)
Tunabaki na tulichonacho kwa kuwa macho na makini muda wote, na kama vile uhuru wa mtu unavyotokana na misingi au hatua kumi na mbili, basi uhuru wa kikundi unatokana na mila kumi na mbili.
Ili mradi vinavyotuunganisha ni imara kuliko vinvyotugawanyisha, yote ni njema.
1. Ustawi wetu wa jumla unabidi uje kwanza ; uponyaji wetu binafsi unategemea umoja wa NA.
2. Kwa ajili ya malengo ya kikundi chetu cha NA kuna mamlaka kuu moja tu - Mungu mwenye upendo kama atakayojionyesha kwetu. Viongozi wetu ni watumishi wanaoaminiwa, hawatawali.
3. Sharti pekee la uanachama ni nia ya kuacha kutumia.
4. Kila kikundi cha NA ni huru isipokuwa kwenye masuala yanayohusu vikundi vingine au NA kwa ujumla.
5. Kila kikundi cha NA kina lengo kuu moja - kufikisha ujumbe kwa mlevi ambaye bado anateswa na ulevi.
6. Kikundi cha NA hakitakiwi kutumia, kufanyia biashara au kuazima jina la NA kwa mradi wowote wa nje, yasije matatizo ya pesa, mali au ufahari yakatuyumbisha kutoka kwenye lengo letu kuu.
7. Kila kikundi cha NA kinabidi kijitegemee, na kukataa misaada ya nje.
8. NA inabidi inbaki milele nje ya mipaka ya kiofisi, lakini vituo vyetu vya huduma vinaweza vikaajiri wafanyakazi maalum.
9. NA, kwa mantiki hiyo hiyo, inabidi isiwe na muundo wa utawala, lakini tunaweza kuunda bodi au kamati za huduma zitakazowajibika moja kwa moja kwa wale inaowatumikia.
10. NA haina maoni kuhusu masuala ya nje; kwa hiyo jina la NA halitakiwi kuhusishwa katika migogoro yoyote ya umma au jamii.
11. Sera yetu ya uhusiano na jamii au umma imelenga zaidi kwenye kuvutia kuliko kwenye kuhamasisha ; ni lazima tukwepe kujitangaza kupitia chapa, redio na filamu.
12. Kutokujulikana ni msingi wa kiroho wa mila zetu zote, ikitukumbusha daima kutanguliza misingi kabla ya watu.
Tunakaribisha maoni, ushauri na maswali.
Narcotics Anonymous (Tanzania)  inakutana kila siku kuanzia saa saba mchana hadi saa nane mchana katika ukumbi wa hoteli ya Itongo, Mtaa wa Msufini, Uwanja wa Fisi, Tandale/Manzese, Dar es Salaam, Tanzania.
Kwa maelezo zaidi wasiliana na edward@maweni.com