NA Tanzania inatimiza mwezi mmoja tangu kuanzishwa. Ilikuwa mnamo tarehe 14 Novemba, 2006, siku ambayo Edward, Khadija na Stephane walianzisha NA Tanzania kwenye bwawa la Maweni, juu ya milima ya Usambara, kaskazini mashariki mwa Tanzania. Shukrani za dhati tunazielekeza kwa utawala na watumishi wa Maweni Farm Ltd, kwa kutengeneza mazingira yaliyowezesha tukio hilo.